Tuesday, August 26, 2008

ZINEDINE YAZID ZIDANE "ZIZOU"




MAISHA YA ZIDANEZidane ni malgeria ambaye alizaliwa ufaransa, wazazi wake walikuwa wanakaa katika jimbo la KABYLIE kijiji cha AGUEMONE na kuhamia ufaransa katika jiji la paris mwaka 1953 na baadaye kuhamia MARSEILLE.
Ambapo tarehe 23 june 1972 zidane alizaliwa katika jiji la marseille na kuepewa jina la utani la ZIZOU.
Kiungo huyu wa zamani wa ufaransa alikuwemo kwenye kikosi ambacho kilitwaa ubingwa wa dunia mwaka 1998 na EURO 2000 na kupata mpira wa dhaabu baada ya kuingoza ufaransa katika kombe la dunia mwaka 2006 katika mechi ambayo alitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumpiga beki wa italy marco materazzi kichwa.
Amecheza club nne na kutwaa club bingwa ulana akiwa na Real Madrid mwaka 2002.
Ni mmoja kati ya wachezaji wawili kuwa wachezaji bora mara tatu mwinine ni RONALDO DE LIMA
Alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa ulaya mwa 1998.
Mwaka 2004 mashabiki walimchagua kuwa UEFA 15 unnversary golden jubilee pull na ni kujumuishwa na pele katika orodha ya wachezaji 100 bora baada ya kustaafu soka mwaka 2006.
Lakini mwaka june 2008 alifanyiwa mahojiano na BBC na kusema kwamba anatamani kurudi kucheza mpira kwani anashughuli yeyote ya kufanya.

AKIWA CANNES & BORDEAUX 1988-1996
Zidane aliaza kucheza mpira katika timu ya vijana ya us saint henri ambayo ni ya mitaani katika jimbo la La Castellane akiwa na umri wa miaka kumi na nne.
As cannos scout Jean Varraud alimchukua na kujiunga na AS CANNES.
Zidane alianza kucheza ligue 1 akiwa na miaka 17 na alifunga goli lake la kwanza 8 february 1991 na akazawadiwa gari na raisi wa timu kwa msimu wa kwanza kwa kuiwezesa cannes kucheza katika kombe la UEFA.
Zidane aliamia BORDEAUX msimu wa mwaka 1992-93 na kushinda kombe la intertoto na kushika nafasi ya pili katika kombe la UEFA.1995-96
Kwamiaka minne alijenga ushirikiano na BIXENTE LIZARAZU na CHRISTOPHE DUGARY ambaye sasa ni afisamasoko wa Bordeux na mwaka 1998 walikuwa wote kwenye timu ya taifa.
Mwaka 1995 kocha mkuu wa b'burn rovers Kenny Dalgish alimueleza mmiliki wa timu kuwa ana taka kumsajili zidane na dugary mmliki wa timu JACK WALKER alimjibu na kusema kwanini zidane wakati tunaye TIM SHEXWOOD.

JUVENTUS
Mwaka 1996 zidane alihamia kwenye club bingwa ya ulaya juventusfc kwa ada ya £3 million.
Zidane alikuwa mchezaji chaguo la kwanza la kocha marcello Lippi na kunyakuwa ubingwa wa scudetto mwaka 1996-97 na ubingwa wa mabara kwa ushindi wa bao 1-0 walilowafunga river plate.
Nakufanikiwa kufika fainaili ya champions league na juventus na kufungwa goli 3-1 na Borussia Dortmund.
Alifunga goli saba katika mechi 32 alizocheza na kuisaidia juvenus kushika nafasi ya pili katika fainali ya club bingwa kwa kufungwa na real madrid kwa goli 1-0.
Mwaka 2000-01 katika ligi ya serie A juve ilimaliza ikiwa nafasi ya pili nyuma kwa poiti 2 kwa mabingwa AS ROMA.
Zidand alitolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kwa kumpiga kichwa mchezaji wa HAMBURGERSV JACHEN KIENTZ mwaka 2000-01.
Alifanikiwa kufunga magoli 24 kwa muda wote aliocheza juve, alifanikiwa kunyakuwa intercontinental cup 1999 na intertoto cup na makombe mawili ya scudetti.

REAL MADRID 2001-06
Mwaka 2001 zidane alijiunga na real madrid kwa €76 milioni na kufanya kuwa mchezaji ghali kuliko wote katika historia ya soka na alisaini mkataba wa miaka minne.
Mwaka 2002 walifanikiwa kunyakua kombe la club bingwa ulaya kwa kuifunga BAYER LEVERKUSEN kwa magoli 2-1 katika jiji la GLASGOW pia walipata kombe la EUROPEAN SUPER CUP na SPANISH SUPER CUP.
2003 zidane alitajwa kuwa mchezaji bora wa dunia wa fifa wa mwaka na kuungana na RONALDO kwa kuwa wachezaji pekee kuwa wachezaji bora mara tatu.
Alifunga hat-trick katika ushindi wa goli 4-2 dhidi ya sevilla.
Zidane aliishia nusu fainali ya kombe la COPA DEL REY na kumi na sita bora ya club bingwa ulaya, na kumaliza ligi ikiwa nyuma kwa pointi 12 kwa BARCELONA.
7 may 2006 zidane alitangaza kustaafu soka kabla ya kucheza mechi ya mwisho ya nyumbani BERNABEU na kutoka sare ya 3-3 na VILLAREAL CF
Na wachezaji wenzake wakiwa na jersey ikiwa imeandikwa "ZIDANE"2001-06.

SOKA LA KIMATAIFA
Zidane alikuwa ni raia wa ufaransa na algeria yeye alipenda kucheza timu ya taifa ya algeria lakini kocha ABDELHAMID KERMALI akumtaka kwenye kikosi chake akidai bado mdogo sana na katika nafasi ya kiungo.
Mwaka 2005 zidane alipinga uvumi wa kuwa awezi kuchezea timu ya taifa ya algeria kwakuwa ameipenda ufaransa.
Mwaka 1998 zidane aliweza kuiongoza ufaransa vizuri na kufanikiwa kutwaa kombe la dunia kwa kuitandika brazil kwa magoli 3-0.
Mwaka 2000 aliiwezesha ufaransa kutwaa kombe la ulaya kwa kuifunga italy
Mwaka 2002 zidane akucheza mechi mbili za makundi katika michuano ya kombe la dunia kwa kuwa majeruhi lakini alicheza mechi ya tatu na kufanya kutolewa katika hatua ya makundi wakiwa hawajafunga goli hata moja.
Mwaka 2006 aliisaidia ufaransa kufika fainali ya kombe la dunia lakini alitolewa nje kwa kadi nyekundu katika dakika ya 110 kwa kumpiga kichwa beki wa italy MARCO MATERAZZI.
Alifunga goli kwa mkwaju wa penati na kumfanya awe mmoja wa wachezaji wanne kufunga katika fainali mbili tofauti wengine ni PELE,VAVA na PAULO BREITNER na PELE VAVA na GEOFT HURST ni wachezaji waliofunga magoli matatu katika fainali za kombe la dunia.

UGOMVI NA MARCO MATERAZZI
Zidane na beki wa italy marco materezzi walikuwa wanaongozana uwanjani lakini zidane alisimama na kumpiga kichwa cha kifua lakini refaree HARACIO EIZONDO akumuona mpaka pale alipopewa taarifa na kamisaa LUIS MEDINA na kupewa kadi nyekundu katika dakika ya 110.

Friday, August 22, 2008

EDISON ARANTES DO NASCIMENTO"PELE"



Pele alizaliwa october 23 1940 huko TRES CORACOES BRAZIL.
Anaurefu wa 1.74m{5ft0.5in}
Alizaliwa na JOAO RAMOS DO NASCIENT mchezaji wa zamani wa FLUMINENSE aliyejulikana kama DENDINHO na MARIA CELESTE ARANTES walimpa jina la inventor wa kimarekani THOMAS EDISON na jina lake la utani alijulikana kama DICO katika familia yake.
Alipata jina la utani la PELE akiwa anasoma shule. Pele aliitwa kutokana na makosa ya kimatamshi lililotokana na jina la golikipa wa zamani wa vasco da gama "BILE" na kulibadilisha na kuitwa "PILE" jina ambalo akulipenda.
Pele alisimamishwa shule kwa kumpiga mwanafunzi mwenzake kwa kumwita jina hilo.
BILE walilipeleka kwenye lugha ya ki irishi na likasomeka PEILE likimaanisha FOOTBAL.
Pele alikulia kwenye maisha ya kimaskini huko Baura Sáo Paulo.
Alijipatia fedha kwa kubrashi viatu vya club ya Baura Athletic kwenye siku za mechi.
Pele alianzakutengeneza mpira wa makaratasi ya magazeti na kamba na kuweka soksi au matunda yaliyokaa kama mpira.
Mwaka 1954 vilabu vya america vilimtamani pele ambaye alijiunga na timu ya Baquinho boys timu ambayo ilikuwa inanolewa na mchezaji wa zamani wa kimataifa wa brazil WALDEMAR DE BRITO ambaye alishiriki kwenye kombe la dunia mwaka 1934 huko italy.
AKIWA SANTOS
Mwaka 1956 DE BRITO alimchukua pele na kumpeleka santos huko sao paul kujaribu soka la kulipwa na club ya santos futebol clube.
Akiwa na miaka 15 alikuwa mchezaji mkubwa duniani.
Akiwa santos pele alifanikiwa kucheza na wachezaji wakubwa sana duniani kama zito pele na coutinho ambao alicheza nao moja mbila na kufunga magoli.
Pele alifanikiwa kufunga goli lake la kwanza akiwa na jezi ya santos tarehe 7 september 1956 katika ushindi wa goli 7-1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Corinthians.
Wakati unaanza mwaka 1957 pele alianza katika timu ya kwanza akiwa na umri wa miaka 16 na kuwa mfungaji bora katika ligi miezi kumi baada ya kusaini mkataba.
Kocha mkuu wa timu ya taifa alimwita kwenye timu ya taifa ya brazil.
Baada ya fainali za kombe la dunia za mwaka 1962 vilabu vikubwa ya ulaya vilitoa ofa ya kumsajili kijana huyu lakini selikari ya brazil ilikataa na kusema pele ni kivutio cha taifa kwahiyo awezi kuondoka nchini mwake.
Nov 19, 1969 pele alifunga goli lake la elfu moja 1000 katika michuano yote ilikuwa dhidi ya vasco da gama kwa njia ya penati katika uwanja wa Maracana na kulidedicate kwa watoto wote wanaoishi kwenye maisha ya kimaskini nchini brazil.
Pele alifunga goli zuri katika uwanja wa compeonato paulistu ilikuwa mechi dhidi ya sao paulo 2, august 1959. Kulikuwa hakuna video iliyochukua mechi hiyo ambayo ilishindwa kuwekwa kwenye computer.
March 1961 pele alifunga goli lililojulikana ka "goal of plague" ilikuwa dhidi ya fluminese katika uwanja wa wa Maracana na kulifanya kuwa goli zuri kuliko yote yaliyo wahi kutokea katika uwanja wa MARACANA.
1967 huko nigeria walisimamisha vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa masaa 48 kwa kumuangalia pele katika mchezo uliofanyika lagos.
NEW YORK COSMOS
Baada ya msimu wa mwaka 1972 akiwa na santos pele alistafu katika club hiyo ya brazil baada ya miaka miwili baadaye pele alijiunga ya New york cosmos ya amerika kaskazini soccer league {NASL} akiwa marekani pele aliweza kufunga magoli ya ticktack au bicycle kick na kusababisha watu wengi wafungulie kituo cha tv cha michezo cha sports tv series, ABC'S wide world of sport.
Oct.1.1977 pele alicheza mechi yake ya mwisho ya kumuaga kati ya cosmos na santos. Santos walikuja New york na New jersey na kuibuka na ushindi wa goli 2-0 mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Giants na kurushwa na kituo cha television cha ABC'S wide world of sports na kuonekana kote duniani.
Baba na mke wake waliudhurha mechi hii.
Kabla ya mechi pele aliutubia na kusena "LOVE" mara tatu.
Kipindi cha kwanza pele alicheza timu ya cosmos na kipindi cha pili alicheza santos.
Reynaldo alifunga goli la kwanza baada ya kumalizia cross.
Pele alifunga goli la pili kwa njia ya adhabu.
Katika kipindi cha mapumziko pele alivua shirt no 10 na kumpelekea baba yake alisindikizwa na mchezaji mwenzake wa cosmos Ramon Mittlin ambaye alimbadili pele ambaye alifunga goli na kufanya matokeo yawe2-1 na baada ya mechi pele alishika bendela ya marekani mkono wa kulia na bendela ya brazil mkono wa kushoto.
Wakati anacheza mpira alijulikana kam MFALME WA MPIRA{o rei do futebol} MFALME PELE {o rei pele}
Aliitwa kwenye timu ya taifa akiwa na umri wa miaka 16 na kunyakua kombe la dunia akiwa na umri wa miaka 17.
Muda wote aliokuwa anacheza pele alikuwa mfungaji bora katika timu ya taifa ya brazil.
Na ni mchezaji pekee kushinda makombe matatu ya kombe la dunia.
Mwaka 1962 alijumuishwa kwenye kikosi cha brazil na alipata majeruhi na kufanya asipewe medali.
Nov 2007 FIFA walitangaza kwamba anastahili kupata medali ya mwaka 1962. Na kumfanya awe mchezaji peke kutwaa medali ya kombe la dunia.
Tangu amestaafu 1977 pele amekuwa balozi wa mpira katika FIFA na kivutio cha serikali ya brazil.
Pia alichaguliwa kuwa mchezaji wa karne na kupewa tuzo na international olympic committee.